Zaburi 38:1-11
Zaburi 38
Maombi Ya Mtu Anayeteseka
Zaburi ya Daudi. Maombi.
38:1 Za 6:1Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako,
wala kuniadhibu katika ghadhabu yako.
38:2 Ay 6:4Kwa kuwa mishale yako imenichoma,
na mkono wako umenishukia.
38:3 Mit 3:8; 4:22; Ay 33:19Hakuna afya mwilini mwangu
kwa sababu ya ghadhabu yako,
mifupa yangu haina uzima
kwa sababu ya dhambi zangu.
38:4 Za 40:12; 65:3; Hes 11:14; Ezr 9:6; Lk 11:46Maovu yangu yamenifunika
kama mzigo usiochukulika.
38:5 Za 147:3; Ay 19:17; Za 69:5; Mit 5:23; 12:23; 13:16; Mhu 10:3Majeraha yangu yameoza na yananuka,
kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
38:6 Za 57:6; 145:14; 146:8; 35:14Nimeinamishwa chini na kushushwa sana,
mchana kutwa nazunguka nikiomboleza.
38:7 Ay 14:22; 7:5Viuno vyangu vimejaa maumivu yaunguzayo,
hakuna afya mwilini mwangu.
38:8 Za 6:3, 6; 22:1; 34:18; Mit 17:22; 5:11Nimedhoofika na kupondwa kabisa,
nasononeka kwa maumivu makuu ya moyoni.
38:9 Za 119:20; 143:7; Ay 3:24Ee Bwana, yote ninayoyaonea shauku
yako wazi mbele zako,
kutamani kwangu sana
hakufichiki mbele zako.
38:10 Ay 37:1; Za 6:7; 31:10; 19:8; 88:9Moyo wangu unapigapiga,
nguvu zangu zimeniishia;
hata macho yangu yametiwa giza.
38:11 Za 38:5; Lk 10:31Rafiki na wenzangu wananikwepa
kwa sababu ya majeraha yangu;
majirani zangu wanakaa mbali nami.