Zaburi 37:10-20 NEN

Zaburi 37:10-20

37:10 Ay 7:10; Eze 27:30Bado kitambo kidogo, nao waovu hawataonekana,

ingawa utawatafuta, hawataonekana.

37:11 Hes 6:26; 14:24; Mt 5:5; Law 26:6Bali wanyenyekevu watairithi nchi

na wafurahie amani tele.

37:12 Ay 16:9; Za 2:1; 31:13; 35:16; 112:10Waovu hula njama dhidi ya wenye haki

na kuwasagia meno,

37:13 1Sam 26:10; Za 11:2; 35:10; 22:20; Eze 12:23bali Bwana huwacheka waovu,

kwa sababu anajua siku yao inakuja.

37:14 Za 22:20; 11:2; 35:10Waovu huchomoa upanga

na kupinda upinde,

ili wawaangushe maskini na wahitaji,

kuwachinja wale ambao njia zao ni nyofu.

37:15 1Sam 2:4; Yer 49:35; Za 9:16; 46:9Lakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe,

na pinde zao zitavunjwa.

37:16 Mit 15:16; 16:8; 1Tim 6:6Bora kidogo walicho nacho wenye haki

kuliko wingi wa mali wa waovu wengi;

37:17 Za 10:15; 41:12; 140:12; 145:14; 146:7; Ay 38:15kwa maana nguvu za waovu zitavunjwa,

lakini Bwana humtegemeza mwenye haki.

37:18 Ay 23:10; Za 44:21; 37:27, 29Bwana anazifahamu siku za wanyofu,

na urithi wao utadumu milele.

37:19 Ay 5:20Siku za maafa hawatanyauka,

siku za njaa watafurahia wingi wa vitu.

37:20 Za 34:21; 68:2; 102:3; Isa 51:6Lakini waovu wataangamia:

Adui za Bwana watakuwa

kama uzuri wa mashamba,

watatoweka,

watatoweka kama moshi.

Read More of Zaburi 37