Zaburi 37:10-20
37:10 Ay 7:10; Eze 27:30Bado kitambo kidogo, nao waovu hawataonekana,
ingawa utawatafuta, hawataonekana.
37:11 Hes 6:26; 14:24; Mt 5:5; Law 26:6Bali wanyenyekevu watairithi nchi
na wafurahie amani tele.
37:12 Ay 16:9; Za 2:1; 31:13; 35:16; 112:10Waovu hula njama dhidi ya wenye haki
na kuwasagia meno,
37:13 1Sam 26:10; Za 11:2; 35:10; 22:20; Eze 12:23bali Bwana huwacheka waovu,
kwa sababu anajua siku yao inakuja.
37:14 Za 22:20; 11:2; 35:10Waovu huchomoa upanga
na kupinda upinde,
ili wawaangushe maskini na wahitaji,
kuwachinja wale ambao njia zao ni nyofu.
37:15 1Sam 2:4; Yer 49:35; Za 9:16; 46:9Lakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe,
na pinde zao zitavunjwa.
37:16 Mit 15:16; 16:8; 1Tim 6:6Bora kidogo walicho nacho wenye haki
kuliko wingi wa mali wa waovu wengi;
37:17 Za 10:15; 41:12; 140:12; 145:14; 146:7; Ay 38:15kwa maana nguvu za waovu zitavunjwa,
lakini Bwana humtegemeza mwenye haki.
37:18 Ay 23:10; Za 44:21; 37:27, 29Bwana anazifahamu siku za wanyofu,
na urithi wao utadumu milele.
37:19 Ay 5:20Siku za maafa hawatanyauka,
siku za njaa watafurahia wingi wa vitu.
37:20 Za 34:21; 68:2; 102:3; Isa 51:6Lakini waovu wataangamia:
Adui za Bwana watakuwa
kama uzuri wa mashamba,
watatoweka,
watatoweka kama moshi.