Zaburi 37:1-9 NEN

Zaburi 37:1-9

Zaburi 3737 Zaburi hii imetungwa kila beti likianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22.

Mwisho Wa Mwovu Na Urithi Wa Mwenye Haki

Zaburi ya Daudi.

37:1 Mit 3:31; 3:17, 18; 24:19Usisumbuke kwa ajili ya watendao maovu,

wala usiwaonee wivu watendao mabaya,

37:2 2Fal 19:26; Ay 14:2; Za 92:7; 102:4; 90:6; Yak 1:10; Isa 40:7; Za 37:38kwa maana kama majani watanyauka mara,

kama mimea ya kijani watakufa mara.

37:3 Kum 30:20; Yn 10:9; Eze 34:14Mtumaini Bwana na utende yaliyo mema;

Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.

37:4 Ay 27:10; 7:6; Wim 2:3; Za 21:2; 145:19; Mit 6:33; Isa 58:14; 1Pet 1:8Jifurahishe katika Bwana

naye atakupa haja za moyo wako.

37:5 Za 4:5; 57:10; Mt 6:25; 1Pet 5:7Mkabidhi Bwana njia yako,

mtumaini yeye, naye atatenda hili:

37:6 Ay 11:8; 7:20; 11:17; Rum 11:33; Za 145:9; 18:24; 103:17; 112:3; Mik 7:9Yeye atafanya haki yako ingʼae kama mapambazuko,

na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri.

37:7 Kut 14:14; Yer 12:1; Isa 41:1; 38:13; Za 119:150; 40:1; 27:14; 21:11; 26:10; 130:5; Hab 3:16; Rum 8:25Tulia mbele za Bwana

na umngojee kwa uvumilivu;

usisumbuke watu wanapofanikiwa katika njia zao,

wanapotekeleza mipango yao miovu.

37:8 Efe 4:26, 31; Ay 5:2; Kol 3:8; Mit 14:29; Za 73:3; Yak 1:19Epuka hasira na uache ghadhabu,

usihangaike: itakuongoza tu kutenda uovu.

37:9 Za 31:22; 101:8; 25:13; Mit 2:22; Isa 57:13; 40:31; 51:5, 22; 49:8, 23; 25:9; 26:8; Mt 5:5Kwa maana waovu watakatiliwa mbali,

bali wale wanaomtumaini Bwana watairithi nchi.

Read More of Zaburi 37