Zaburi 35:1-10
Zaburi 35
Kuomba Msaada: Kuokolewa Kutokana Na Maadui
Zaburi ya Daudi.
35:1 1Sam 24:15; Kut 14:14Ee Bwana, pingana na wale wanaopingana nami,
upigane na hao wanaopigana nami.
35:2 Za 3:3, 7; Ay 17:3; Mwa 50:24; 35:3; Hes 25:7; Za 27:1; Yos 8:18Chukua ngao na kigao.
Inuka unisaidie.
Inua mkuki wako na fumo35:3 Fumo ni sawa na sagai, maana yake ni mkuki mfupi. lako
dhidi ya hao wanaonifuatia.
Iambie nafsi yangu,
“Mimi ni wokovu wako.”
35:4 Za 38:12; 40:14; 69:6, 19; 70:2; 83:17; 25:3; 129:5; Yer 4:30; Mal 2:9; Isa 45:16Wafedheheshwe na waaibishwe
wale wanaotafuta uhai wangu.
Wanaofanya shauri kuniangamiza
warudishwe nyuma kwa hofu.
35:5 Ay 13:25; Za 1:4; 34:7Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo,
malaika wa Bwana akiwafukuza.
Njia yao na iwe giza na ya utelezi,
malaika wa Bwana akiwafuatilia.
35:7 Ay 18:8; 9:31; Za 7:4; 7:15; 55:23Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu,
na bila sababu wamenichimbia shimo,
35:8 Isa 47:11; 1The 5:3; Za 7:15; Mit 5:22maafa na yawapate ghafula:
wavu walionifichia na uwatege wenyewe,
na waanguke katika shimo hilo,
kwa maangamizo yao.
35:9 Za 2:11; 9:14; 13:5; 27:1; Lk 1:47; 1Sam 2:1; Isa 61:10; Ebr 3:18Ndipo nafsi yangu itashangilia katika Bwana
na kuufurahia wokovu wake.
35:10 Kut 9:14; Za 12:5; 71:19; 18:17, 31; 113:5; 37:14; 86:1; 74:21; 109:16; 140:12; Isa 41:17Nitapaza sauti yangu nikisema,
“Ni nani aliye kama wewe, Ee Bwana?
Wewe huwaokoa maskini kutokana na wale walio na nguvu kuliko wao,
maskini na mhitaji kutokana na wanaowanyangʼanya!”