Zaburi 34:11-22 NEN

Zaburi 34:11-22

34:11 Za 66:16; 32:8; 19:9Njooni, watoto wangu, mnisikilize,

nitawafundisha kumcha Bwana.

34:12 Mhu 3:13; 1Pet 3:10Yeyote kati yenu anayependa uzima

na kutamani kuziona siku nyingi njema,

34:13 1Pet 2:22; Za 39:1; 141:3; Mit 13:3; 21:23; Yak 1:26; Za 12:2basi auzuie ulimi wake na mabaya,

na midomo yake kutokana na kusema uongo.

34:14 Za 37:27; Isa 1:17; 3Yn 11; Rum 14:19Aache uovu, atende mema,

aitafute amani na kuifuatilia.

34:15 Ay 36:7; 23:10; Mal 3:16; Yn 9:31; Za 33:18Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki,

na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.

34:16 Law 17:10; Za 9:6; Yer 23:30; 44:11; Mit 10:7; Kut 17:14; 1Pet 3:10-12Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu,

ili kufuta kumbukumbu lao duniani.

34:17 Za 145:19Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia,

huwaokoa katika taabu zao zote.

34:18 Kum 4:7; Za 51:17; 119:151; 145:18; 109:16; 147:3; Isa 50:8; 61:1Bwana yu karibu na waliovunjika moyo,

na huwaokoa waliopondeka roho.

34:19 Za 34:17; 25:17; Ay 5:19; 2Tim 3:11Mwenye haki ana mateso mengi,

lakini Bwana humwokoa nayo yote,

34:20 Yn 19:34huhifadhi mifupa yake yote,

hata mmoja hautavunjika.

34:21 Za 7:9; 9:16; 37:20; 73:27; 94:23; 106:43; 112:10; 140:11; Mit 14:32; 24:16Ubaya utamuua mtu mwovu,

nao adui za mwenye haki watahukumiwa.

34:22 Kut 6:6; 15:13; Lk 1:68; Ufu 14:3; Za 2:12; 103:4; 2Sam 4:9Bwana huwakomboa watumishi wake,

yeyote anayemkimbilia yeye

hatahukumiwa kamwe.

Read More of Zaburi 34