Zaburi 34:1-10 NEN

Zaburi 34:1-10

Zaburi 3434 Zaburi hii imetungwa kila mstari ukianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22.

Sifa Na Wema Wa Mungu

Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka.

34:1 Za 71:6; Efe 5:20; 1The 5:18Nitamtukuza Bwana nyakati zote,

sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.

34:2 Za 44:8; 69:32; 107:42; 119:74; Yer 9:24; 1Kor 1:31Nafsi yangu itajisifu katika Bwana,

walioonewa watasikia na wafurahi.

34:3 Za 63:3; 86:12; Dan 4:37; Kut 15:2; Yn 17:1; Rum 15:6Mtukuzeni Bwana pamoja nami,

naam, na tulitukuze jina lake pamoja.

34:4 Za 18:6; 77:2; 18:43; 22:4; 56:13; 86:13; Kut 32:11; Yon 2:2; Mt 7:7; Lk 11:9Nilimtafuta Bwana naye akanijibu,

akaniokoa kwenye hofu zangu zote.

34:5 Kut 34:29; Za 25:3; 44:15; 69:7; 83:16Wale wamtazamao hutiwa nuru,

nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.

34:6 Za 25:17; 2Sam 22:1Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia,

akamwokoa katika taabu zake zote.

34:7 Mwa 32:1; Ebr 1:14; Dan 3:28; 6:22; Mt 18:10; Isa 31:5; Za 22:4; 37:40; 41:1; 97:10; Mdo 12:11; 2Fal 16:17Malaika wa Bwana hufanya kituo

akiwazunguka wale wamchao,

naye huwaokoa.

34:8 Ebr 6:5; 1Pet 2:3; Za 2:12Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema,

heri mtu yule anayemkimbilia.

34:9 Flp 4:19; Za 23:1; Kum 6:13; Ufu 14:7Mcheni Bwana enyi watakatifu wake,

kwa maana wale wamchao

hawapungukiwi na chochote.

34:10 Za 23:1Wana simba wenye nguvu

hutindikiwa na kuona njaa,

bali wale wamtafutao Bwana

hawatakosa kitu chochote kilicho chema.

Read More of Zaburi 34