Zaburi 33:12-22 NEN

Zaburi 33:12-22

33:12 Za 144:15; 65:4; 4:3; 84:4; Kum 7:6; Kut 8:22; 34:9Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao,

watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.

33:13 Za 53:2; 102:19; 11:4; 14:2; Ebr 4:13; 2Nya 16:9; Ay 28:24Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini

na kuwaona wanadamu wote;

33:14 Law 15:31; 1Fal 8:39kutoka maskani mwake huwaangalia

wote wakaao duniani:

33:15 Ay 10:8; 11:11; 10:4; Yer 32:19; Isa 64:8; Hes 7:2; Za 44:21; 119:73; Mit 24:12yeye ambaye huumba mioyo yao wote,

ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.

33:16 1Sam 14:6Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake;

hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.

33:17 Za 20:7Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu,

licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.

33:18 Kut 3:16; Ay 36:7; Za 11:4; 6:4; 34:15; 1Pet 3:12Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao,

kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,

33:19 Za 56:13; Ay 5:20; Mdo 12:11ili awaokoe na mauti,

na kuwahifadhi wakati wa njaa.

33:20 Za 27:14Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini,

yeye ni msaada wetu na ngao yetu.

33:21 1Sam 2:1; Yoe 2:23; Za 30:4; 99:3Mioyo yetu humshangilia,

kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.

33:22 Za 6:4Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana,

tunapoliweka tumaini letu kwako.

Read More of Zaburi 33