Zaburi 33:12-22
33:12 Za 144:15; 65:4; 4:3; 84:4; Kum 7:6; Kut 8:22; 34:9Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao,
watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
33:13 Za 53:2; 102:19; 11:4; 14:2; Ebr 4:13; 2Nya 16:9; Ay 28:24Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini
na kuwaona wanadamu wote;
33:14 Law 15:31; 1Fal 8:39kutoka maskani mwake huwaangalia
wote wakaao duniani:
33:15 Ay 10:8; 11:11; 10:4; Yer 32:19; Isa 64:8; Hes 7:2; Za 44:21; 119:73; Mit 24:12yeye ambaye huumba mioyo yao wote,
ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
33:16 1Sam 14:6Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake;
hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
33:17 Za 20:7Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu,
licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
33:18 Kut 3:16; Ay 36:7; Za 11:4; 6:4; 34:15; 1Pet 3:12Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao,
kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
33:19 Za 56:13; Ay 5:20; Mdo 12:11ili awaokoe na mauti,
na kuwahifadhi wakati wa njaa.
33:20 Za 27:14Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini,
yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
33:21 1Sam 2:1; Yoe 2:23; Za 30:4; 99:3Mioyo yetu humshangilia,
kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
33:22 Za 6:4Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana,
tunapoliweka tumaini letu kwako.