Zaburi 33:1-11 NEN

Zaburi 33:1-11

Zaburi 33

Ukuu Na Wema Wa Mungu

33:1 Za 64:10; 101:1; 147:1; 11:7Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki;

kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.

33:2 Mwa 4:21; 1Kor 14:7; Ufu 5:8; Za 92:3; 144:9Msifuni Bwana kwa kinubi,

mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.

33:3 Za 40:3; 35:27; 47:1; Isa 42:10; Ufu 5:9; Ay 3:7Mwimbieni wimbo mpya;

pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.

33:4 Ufu 19:9; 22:6; Za 19:8; 18:25; 119:142; 25:10Maana neno la Bwana ni haki na kweli,

ni mwaminifu kwa yote atendayo.

33:5 Za 11:7; 6:4Bwana hupenda uadilifu na haki;

dunia imejaa upendo wake usiokoma.

33:6 Ebr 11:3; Kut 8:19; Mwa 1:3, 16; 2Nya 2:12; Yn 1:1-3; Ay 26:13Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa,

jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.

33:7 Mwa 1:10; Yos 3:16Ameyakusanya maji ya bahari

kama kwenye chungu;

vilindi vya bahari

ameviweka katika ghala.

33:8 Kum 6:13; 14:23; Za 2:11; 49:1; Isa 18:3; Mik 1:2Dunia yote na imwogope Bwana,

watu wote wa dunia wamche.

33:9 Za 148:5; Mwa 1:3Kwa maana Mungu alisema, na ikawa,

aliamuru na ikasimama imara.

33:10 Isa 44:25; Za 2:1; Ay 5:12Bwana huzuia mipango ya mataifa,

hupinga makusudi ya mataifa.

33:11 Hes 23:19; Yer 51:12, 29; Ay 23:13; Mit 19:21; Eze 38:10; Mdo 4:27, 28Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele,

makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.

Read More of Zaburi 33