Zaburi 31:9-18
31:9 Za 4:1; 6:7; 63:1Ee Bwana unihurumie, kwa kuwa niko kwenye shida;
macho yangu yanafifia kwa huzuni,
nafsi yangu na mwili wangu kwa sikitiko.
31:10 Za 6:6; 22:5; 32:4; 38:10; 73:26; 25:18; 6:2Maisha yangu yamedhoofika kwa majonzi,
naam, miaka yangu kwa kulia kwa maumivu makali;
nguvu zangu zinaisha kwa ajili ya mateso,
na mifupa yangu inachakaa.
31:11 Kum 30:7; Za 3:7; 25:19; 102; 22:6; 38:11; 88:8Kwa sababu ya adui zangu wote,
nimedharauliwa kabisa na jirani zangu,
hata kwa rafiki zangu nimekuwa tisho,
wale wanionao barabarani hunikimbia.
31:12 Za 28:1; 88:4Nimesahaulika miongoni mwao kama mtu aliyekufa,
nimekuwa kama chombo cha mfinyanzi kilichovunjika.
31:13 Law 19:16; Isa 13:8; Za 50:20; 41:7; 56:6; 71:10; 83:3; Ay 18:11; Yer 6:25; 20:3, 10; 46:5; 49:5; Mao 2:22; Mwa 37:18; Mt 12:14; 27:1Kwa maana nimesikia maneno niliyosingiziwa na wengi;
vitisho viko pande zote;
kwa kuwa wamefanya mashauri dhidi yangu,
na kula njama kuniua.
31:14 Za 4:5Lakini mimi ninakutumaini wewe peke yako, Ee Bwana;
nimesema, “Wewe ndiwe Mungu wangu.”
31:15 Ay 14:5Siku za maisha yangu ziko mikononi mwako,
uniokoe mikononi mwa adui zangu
na wale wanifuatiao.
31:16 Hes 6:25; Dan 9:17; Za 4:6; 6:4Mwangazie mtumishi wako uso wako,
uniokoe kwa ajili ya upendo wako usiokoma.
31:17 Za 22:5; 94:17; 115:17; 25:2; 1Sam 2:9Usiniache niaibike, Ee Bwana,
kwa maana nimekulilia wewe,
bali waovu waaibishwe
na kunyamazishwa Kuzimu.
31:18 Za 120:2; 12:3; Mit 10:18; 26:24; 1Sam 2:3; Yud 15Midomo yao isemayo uongo na inyamazishwe,
kwa maana kwa kiburi na dharau
wao husema kwa majivuno
dhidi ya wenye haki.