Zaburi 27:7-14 NEN

Zaburi 27:7-14

27:7 Za 4:1; 5:3; 18:6; 55:17; 119:149; 130:2; Isa 28:23Isikie sauti yangu nikuitapo, Ee Bwana,

unihurumie na unijibu.

27:8 1Nya 16:11Moyo wangu unasema kuhusu wewe,

“Utafute uso wake!”

Uso wako, Bwana “Nitautafuta.”

27:9 Za 2:5; 119:8; 18:46; 22:24; 37:28; Mwa 49:25; Kum 31:17; 33:29; 4:31; Isa 41:17; 62:12; Yer 14:9Usinifiche uso wako,

usimkatae mtumishi wako kwa hasira;

wewe umekuwa msaada wangu.

Usinikatae wala usiniache,

Ee Mungu Mwokozi wangu.

Hata kama baba yangu na mama wakiniacha,

Bwana atanipokea.

27:11 Ezr 8:21; Za 5:8; 72:4; 78:42; 106:10; Yer 21:12; Kut 33:13Nifundishe njia yako, Ee Bwana,

niongoze katika njia iliyonyooka

kwa sababu ya watesi wangu.

27:12 Kum 19:16; Mt 26:60; Mdo 6:13; 1Kor 15:15Usiniachilie kwa nia za adui zangu,

kwa maana mashahidi wa uongo

wameinuka dhidi yangu,

wakipumua ujeuri.

27:13 Kut 33:19; 2Nya 6:41; Za 33:6; 31:19; 145:7; Ay 18:13Nami bado nina tumaini hili:

nitauona wema wa Bwana

katika nchi ya walio hai.

27:14 Efe 6:10; Amu 5:21; Kum 1:21; Sef 3:8; Hab 2:3; Za 33:20; 130:5, 6; Mdo 1:4; Isa 8:17; 30:18Mngojee Bwana,

uwe hodari na mwenye moyo mkuu,

nawe, umngojee Bwana.

Read More of Zaburi 27