Zaburi 27:1-6
Zaburi 27
Sala Ya Kusifu
Zaburi ya Daudi.
27:1 2Sam 22:29; Ay 13:5; Za 3:8; 9:9; 56:4, 11; 118:6; Kut 15:2Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu,
nimwogope nani?
Bwana ni ngome ya uzima wangu,
nimhofu nani?
27:2 Za 9:3; 20:8; 37:24; Dan 11:19; Rum 11:11Waovu watakaposogea dhidi yangu
ili wanile nyama yangu,
adui zangu na watesi wangu watakaponishambulia,
watajikwaa na kuanguka.
27:3 Mwa 4:7; Za 3:6; Ay 4:6Hata jeshi linizunguke pande zote,
moyo wangu hautaogopa;
hata vita vitokee dhidi yangu,
hata hapo nitakuwa na ujasiri.
27:4 Lk 10:42; Za 23:6; 61:4Jambo moja ninamwomba Bwana,
hili ndilo ninalolitafuta:
niweze kukaa nyumbani mwa Bwana
siku zote za maisha yangu,
niutazame uzuri wa Bwana
na kumtafuta hekaluni mwake.
27:5 Ay 38:23; Za 12:7, 8; 40:2Kwa kuwa siku ya shida,
atanihifadhi salama katika maskani yake,
atanificha uvulini mwa hema yake
na kuniweka juu kwenye mwamba.
27:6 2Sam 22:49; Za 3:3; 33:2; 54:6; 18:48; 22:12; 92:1; 50:14; 107:22; 116:17; 147:7; Ezr 3:13; Ay 22:26; Kut 15:1; Efe 5:19Kisha kichwa changu kitainuliwa
juu ya adui zangu wanaonizunguka.
Katika maskani yake nitatoa dhabihu kwa kelele za shangwe;
nitamwimbia Bwana na kumsifu.