Zaburi 22:1-11
Zaburi 22
Kilio Cha Uchungu Na Wimbo Wa Sifa
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi.
22:1 Za 9:10; 10:1; Mt 27:46; Ay 3:24; 6:15; Mk 15:34; Ebr 5:7Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa?
Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
22:2 Ay 19:7; Za 42:3; 88:1Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu,
hata usiku, sinyamazi.
22:3 2Fal 19:22; Za 71:22; 148:14; Mk 1:24; Ufu 4:8; Kut 15:2; Isa 6:3Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu;
wewe ni sifa ya Israeli.22:3 Tafsiri zingine zinasema: uketiye juu ya sifa za Israeli.
22:4 Za 78:53; 107:6Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao,
walikutumaini nawe ukawaokoa.
22:5 1Nya 5:20; Rum 9:33; Za 25:3; 31:17; 71:1; 2Nya 13:18; Isa 8:17; 25:9; 26:3; 30:18; 49:23Walikulilia wewe na ukawaokoa,
walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
22:6 Ay 4:19; Mt 16:21; Mal 2:9; Isa 60:14; 49:7; 53:3; Za 119:141; 64:8; 109:25; 69:19; 2Sam 12:14Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu,
wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
22:7 Mt 9:24; 27:41; Mk 15:20, 29, 31, 32; Lk 16:14; 23:36, 39; Mt 27:39, 44; Ay 17:2; Za 35:16; 69:12; 74:18Wote wanionao hunidhihaki,
hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
22:8 Za 91:14; 3:2; 2Sam 22:20; Mt 3:17; 27:43Husema, “Anamtegemea Bwana,
basi Bwana na amwokoe.
Amkomboe basi, kwa maana
anapendezwa naye.”
22:9 Ay 10:18; Hes 1:7; Za 71:6; 78:7Hata hivyo ulinitoa tumboni,
ukanifanya nikutegemee,
hata nilipokuwa ninanyonya
matiti ya mama yangu.
22:10 Za 71:6; Isa 46:3; 49:1Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa,
toka tumboni mwa mama yangu
umekuwa Mungu wangu.
22:11 Za 10:1, 14; 2Fal 14:26; Isa 41:28Usiwe mbali nami,
kwa maana shida iko karibu
na hakuna wa kunisaidia.