Zaburi 22:1-11 NEN

Zaburi 22:1-11

Zaburi 22

Kilio Cha Uchungu Na Wimbo Wa Sifa

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi.

22:1 Za 9:10; 10:1; Mt 27:46; Ay 3:24; 6:15; Mk 15:34; Ebr 5:7Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?

Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa?

Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?

22:2 Ay 19:7; Za 42:3; 88:1Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu,

hata usiku, sinyamazi.

22:3 2Fal 19:22; Za 71:22; 148:14; Mk 1:24; Ufu 4:8; Kut 15:2; Isa 6:3Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu;

wewe ni sifa ya Israeli.22:3 Tafsiri zingine zinasema: uketiye juu ya sifa za Israeli.

22:4 Za 78:53; 107:6Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao,

walikutumaini nawe ukawaokoa.

22:5 1Nya 5:20; Rum 9:33; Za 25:3; 31:17; 71:1; 2Nya 13:18; Isa 8:17; 25:9; 26:3; 30:18; 49:23Walikulilia wewe na ukawaokoa,

walikutegemea wewe nao hawakuaibika.

22:6 Ay 4:19; Mt 16:21; Mal 2:9; Isa 60:14; 49:7; 53:3; Za 119:141; 64:8; 109:25; 69:19; 2Sam 12:14Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu,

wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.

22:7 Mt 9:24; 27:41; Mk 15:20, 29, 31, 32; Lk 16:14; 23:36, 39; Mt 27:39, 44; Ay 17:2; Za 35:16; 69:12; 74:18Wote wanionao hunidhihaki,

hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:

22:8 Za 91:14; 3:2; 2Sam 22:20; Mt 3:17; 27:43Husema, “Anamtegemea Bwana,

basi Bwana na amwokoe.

Amkomboe basi, kwa maana

anapendezwa naye.”

22:9 Ay 10:18; Hes 1:7; Za 71:6; 78:7Hata hivyo ulinitoa tumboni,

ukanifanya nikutegemee,

hata nilipokuwa ninanyonya

matiti ya mama yangu.

22:10 Za 71:6; Isa 46:3; 49:1Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa,

toka tumboni mwa mama yangu

umekuwa Mungu wangu.

22:11 Za 10:1, 14; 2Fal 14:26; Isa 41:28Usiwe mbali nami,

kwa maana shida iko karibu

na hakuna wa kunisaidia.

Read More of Zaburi 22