Zaburi 21:8-13
21:8 Isa 10:10Mkono wako utawashika adui zako wote,
mkono wako wa kuume utawakamata adui zako.
21:9 Kum 32:22; Yer 15:14Wakati utakapojitokeza
utawafanya kama tanuru ya moto.
Katika ghadhabu yake Bwana atawameza,
moto wake utawateketeza.
21:10 Kum 28:18Utawaangamiza wazao wao kutoka duniani,
uzao wao kutoka wanadamu.
21:11 Za 2:1; 10:2; 26:10; 37:7; Ay 10:3Ingawa watapanga mabaya dhidi yako
na kutunga hila, hawawezi kufanikiwa,
21:12 Kut 23:27kwa kuwa utawafanya wakimbie
utakapowalenga usoni pao
kwa mshale kutoka kwenye upinde wako.
21:13 Za 18:46; Ufu 15:3, 4Ee Bwana, utukuzwe katika nguvu zako,
tutaimba na kusifu nguvu zako.