Zaburi 19:7-14
19:7 Yak 1:25; Kum 4:6; Za 1:2; 23:3; 93:5; 119:130, 138, 142, 144; 11:7Sheria ya Bwana ni kamilifu,
ikihuisha nafsi.
Shuhuda za Bwana ni za kuaminika,
zikimpa mjinga hekima.
19:8 Za 33:4; 38:10; 119:14, 128; Ezr 9:7; Neh 9:13; Rum 7:12Maagizo ya Bwana ni kamili,
nayo hufurahisha moyo.
Amri za Bwana huangaza,
zatia nuru machoni.
19:9 Mhu 12:13; Isa 33:6; Za 34:11; 111:10; 119:138; Mit 1:7Kumcha Bwana ni utakatifu,
nako kwadumu milele.
Amri za Bwana ni za hakika,
nazo zina haki.
19:10 Ay 22:24; Eze 3:3; Mit 8:10; 1Sam 14:27; Za 119:72, 103Ni za thamani kuliko dhahabu,
kuliko dhahabu iliyo safi sana,
ni tamu kuliko asali,
kuliko asali kutoka kwenye sega.
19:11 Mit 6:22Kwa hizo mtumishi wako anaonywa,
katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
19:12 Za 51:2; 90:8; Mhu 12:14Ni nani awezaye kutambua makosa yake?
Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
19:13 Hes 15:30; Mwa 6:9; Za 18:32; 119:133Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi,
nazo zisinitawale.
Ndipo nitakapokuwa sina lawama,
wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
19:14 Za 104:34; 18:31; Kut 6:6; Isa 44:6; Ay 19:25Maneno ya kinywa changu
na mawazo ya moyo wangu,
yapate kibali mbele zako, Ee Bwana,
Mwamba wangu na Mkombozi wangu.