Zaburi 18:37-42
18:37 Law 26:7Niliwafuatia adui zangu na nikawapata,
sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
18:38 Za 68:21; 110:6; 36:12; 47:3; 140:10; Isa 26:14Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena;
walianguka chini ya miguu yangu.
18:39 Za 18:32, 47; Isa 45:5, 24; Za 47:3; 144:2Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita;
uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
18:40 Yos 7:12; Za 18:37Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia,
nami nikawaangamiza adui zangu.
18:41 2Fal 14:26; Za 50:22; 1Sam 8:18; 14:37; Yer 11:11; Mit 1:28Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa;
walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
18:42 Kum 9:21; Isa 2:22Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo;
niliwamwaga nje kama tope barabarani.