Zaburi 18:25-36
18:25 Za 31:23; 37:23; 50:5; 25:10; 40:11; 89:24; 146:6; Mit 2:8; Mt 18:32-35Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu,
kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
18:26 Mit 15:26; Mt 5:8; Flp 1:10; 1Tim 5:22; Tit 1:15; 1Yn 3:3; Mit 3:34; Mt 10:16; Lk 16:8; Law 26:23Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu,
lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
18:27 2Nya 33:23; Mt 23:12; Ay 41:34; Za 10:5; Mit 3:33-35; 6:17Wewe huwaokoa wanyenyekevu,
lakini huwashusha wenye kiburi.
18:28 1Fal 11:36; Za 132:17; Ay 29:3; Za 97:11; 112:4; Yn 1:5; Mdo 26:18; 2Kor 4:6; 2Pet 1:19; Ay 18:6Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka;
Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
18:29 Isa 45:5; Ebr 11:34Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi,
nikiwa pamoja na Mungu wangu
nitaweza kuruka ukuta.
18:30 Kum 32:4; Za 12:6; 3:3; 2:12; Mit 30:5; Ufu 15:3; Rum 12:3Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu,
neno la Bwana halina dosari.
Yeye ni ngao kwa wote
wanaokimbilia kwake.
18:31 Kum 4:5; 32:39; Za 35:10; 86:8; 89:6; Isa 46:9; 44:6, 8; 45:5, 6, 14, 18, 21; Mwa 49:24Kwa maana ni nani aliye Mungu
zaidi ya Bwana?
Ni nani aliye Mwamba
isipokuwa Mungu wetu?
18:32 1Pet 5:10; Yak 3:2; Za 15:2; 19:13; Ebr 10:14Mungu ndiye anivikaye nguvu
na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
18:33 Za 42:1; Mit 5:19; Isa 35:6; Hab 3:19; Kum 32:13Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu,
huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
18:34 Za 144:1Huifundisha mikono yangu kupigana vita;
mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
18:35 Za 3:5; 37:5, 17; 41:3; 51:2; 54:4; 55:22; 119:116; Isa 41:4, 10, 13; 43:2; 46:4Hunipa ngao yako ya ushindi,
nao mkono wako wa kuume hunitegemeza,
unajishusha chini ili kuniinua.
18:36 Ay 18:7; Za 31:8; 66:9Huyapanua mapito yangu,
ili miguu yangu isiteleze.