Zaburi 18:1-6
Zaburi 18
Wimbo Wa Daudi Wa Ushindi
(2 Samweli 22:1-51)
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi:
18:1 Kut 15:2; Yer 16:19; Kum 32:4; 33:29; Za 91:2; 22:19; 59:9; 81:1; 1Sam 2:2; Isa 2:10; 12:2; 49:5Nakupenda wewe, Ee Bwana,
nguvu yangu.
18:2 Kut 33:22; Isa 2:1; 17:10; Yer 16:19; Za 40:17; 114:2; 2:12; 9:9; 94:20; 28:7, 8; 31:2, 3; 84:9; 119:114; Ebr 2:13; Mwa 15:1; Lk 1:69Bwana ni mwamba wangu,
ngome yangu na mwokozi wangu,
Mungu wangu ni mwamba,
ambaye kwake ninakimbilia.
Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu,
ngome yangu.
18:3 1Nya 16:25; Za 9:13; 76:4Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa,
nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
18:4 Za 116:4; 93:4; 124:6; Eze 43:2; Isa 5:30; 17:12; Yer 6:23; 51:42, 55Kamba za mauti zilinizunguka,
mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
18:5 Mit 14:13Kamba za kuzimu zilinizunguka,
mitego ya mauti ilinikabili.
18:6 Kum 4:30; Za 30:2; 99:6; 102; 120:1; 66:19; 116:1; Ay 16:18Katika shida yangu nalimwita Bwana,
nilimlilia Mungu wangu anisaidie.
Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu,
kilio changu kikafika mbele zake,
masikioni mwake.