Zaburi 17:1-5
Zaburi 17
Sala Ya Mtu Asiye Na Hatia
Sala ya Daudi.
17:1 Za 30:10; 64:1; 80:1; 140:6; 5:1, 2; 39:12; 142:6; 143:1; Isa 29:13Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki,
sikiliza kilio changu.
Tega sikio kwa ombi langu,
halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
17:2 Za 24:5; 26:1; 99:4; Isa 46:13; 50:8-9; 54:17Hukumu yangu na itoke kwako,
macho yako na yaone yale yaliyo haki.
17:3 Za 139:1; Yak 3:2; Ay 7:18; 23:10; Yer 12:3; 50:20Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku,
ingawa umenijaribu, hutaona chochote.
Nimeamua kwamba kinywa changu
hakitatenda dhambi.
17:4 Rum 12:2Kuhusu matendo ya wanadamu:
kwa neno la midomo yako,
nimejiepusha
na njia za wenye jeuri.
17:5 Ay 23:11; Za 44:18; 73:2; 121:3; Kum 32:35Hatua zangu zimeshikamana na njia zako;
nyayo zangu hazikuteleza.