Zaburi 17:1-5 NEN

Zaburi 17:1-5

Zaburi 17

Sala Ya Mtu Asiye Na Hatia

Sala ya Daudi.

17:1 Za 30:10; 64:1; 80:1; 140:6; 5:1, 2; 39:12; 142:6; 143:1; Isa 29:13Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki,

sikiliza kilio changu.

Tega sikio kwa ombi langu,

halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.

17:2 Za 24:5; 26:1; 99:4; Isa 46:13; 50:8-9; 54:17Hukumu yangu na itoke kwako,

macho yako na yaone yale yaliyo haki.

17:3 Za 139:1; Yak 3:2; Ay 7:18; 23:10; Yer 12:3; 50:20Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku,

ingawa umenijaribu, hutaona chochote.

Nimeamua kwamba kinywa changu

hakitatenda dhambi.

17:4 Rum 12:2Kuhusu matendo ya wanadamu:

kwa neno la midomo yako,

nimejiepusha

na njia za wenye jeuri.

17:5 Ay 23:11; Za 44:18; 73:2; 121:3; Kum 32:35Hatua zangu zimeshikamana na njia zako;

nyayo zangu hazikuteleza.

Read More of Zaburi 17