Zaburi 148:7-14
148:7 Za 33:2; 74:13, 14; Mwa 1:21; Isa 43:20; Kum 33:13Mtukuzeni Bwana kutoka duniani,
ninyi viumbe vikubwa vya baharini na vilindi vyote vya bahari,
148:8 Yos 10:11; Ay 37:11, 12; Za 147:15-18; 103:20; Kut 9:18umeme wa radi na mvua ya mawe, theluji na mawingu,
pepo za dhoruba zinazofanya amri zake,
148:9 Isa 44:23; 49:13; 55:12ninyi milima na vilima vyote,
miti ya matunda na mierezi yote,
148:10 Isa 43:20; Hos 2:18wanyama wa mwituni na mifugo yote,
viumbe vidogo na ndege warukao,
148:11 Za 102:15; Mdo 17:28wafalme wa dunia na mataifa yote,
ninyi wakuu na watawala wote wa dunia,
wanaume vijana na wanawali,
wazee na watoto.
148:13 Za 113:2; 138:4; 145:5; 8:1; Isa 6:3; Flp 2:9Wote na walisifu jina la Bwana,
kwa maana jina lake pekee limetukuka,
utukufu wake uko juu ya nchi na mbingu.
148:14 Kut 15:2; 1Pet 2:9; Za 22:3; 145:10; Kum 26:19; Efe 2:17; 1Sam 1:2Amewainulia watu wake pembe,148:14 Pembe hapa inawakilisha mwenye nguvu, yaani mfalme.
sifa ya watakatifu wake wote,
ya Israeli, watu walio karibu na moyo wake.
Msifuni Bwana.