Zaburi 148:7-14 NEN

Zaburi 148:7-14

148:7 Za 33:2; 74:13, 14; Mwa 1:21; Isa 43:20; Kum 33:13Mtukuzeni Bwana kutoka duniani,

ninyi viumbe vikubwa vya baharini na vilindi vyote vya bahari,

148:8 Yos 10:11; Ay 37:11, 12; Za 147:15-18; 103:20; Kut 9:18umeme wa radi na mvua ya mawe, theluji na mawingu,

pepo za dhoruba zinazofanya amri zake,

148:9 Isa 44:23; 49:13; 55:12ninyi milima na vilima vyote,

miti ya matunda na mierezi yote,

148:10 Isa 43:20; Hos 2:18wanyama wa mwituni na mifugo yote,

viumbe vidogo na ndege warukao,

148:11 Za 102:15; Mdo 17:28wafalme wa dunia na mataifa yote,

ninyi wakuu na watawala wote wa dunia,

wanaume vijana na wanawali,

wazee na watoto.

148:13 Za 113:2; 138:4; 145:5; 8:1; Isa 6:3; Flp 2:9Wote na walisifu jina la Bwana,

kwa maana jina lake pekee limetukuka,

utukufu wake uko juu ya nchi na mbingu.

148:14 Kut 15:2; 1Pet 2:9; Za 22:3; 145:10; Kum 26:19; Efe 2:17; 1Sam 1:2Amewainulia watu wake pembe,148:14 Pembe hapa inawakilisha mwenye nguvu, yaani mfalme.

sifa ya watakatifu wake wote,

ya Israeli, watu walio karibu na moyo wake.

Msifuni Bwana.

Read More of Zaburi 148