Zaburi 147:12-20
147:12 Za 48:1Mtukuze Bwana, ee Yerusalemu,
msifu Mungu wako, ee Sayuni,
147:13 Kum 33:25; Law 25:21; Za 128:5; 134:3kwa maana huimarisha makomeo ya malango yako
na huwabariki watu wako walio ndani yako.
147:14 Law 26:6; 2Sam 7:10; Isa 48:18; Za 132:15; Kum 32:14Huwapa amani mipakani mwenu
na kukushibisha kwa ngano safi kabisa.
147:15 Ay 37:12; Za 33:9; 148:5; Isa 55:11Hutuma amri yake duniani,
neno lake hukimbia kasi.
147:16 Za 148:8; Ay 37:12; 38:29Anatandaza theluji kama sufu
na kutawanya umande kama majivu.
147:17 Kut 9:22, 23; Ay 38:22; Za 78:47Huvurumisha mvua yake ya mawe kama changarawe.
Ni nani awezaye kustahimili ukali wa baridi yake?
147:18 Za 33:9; 107:20; 50:3Hutuma neno lake na kuviyeyusha,
huvumisha upepo wake, nayo maji hutiririka.
147:19 Kut 20:1; Mal 4:4; Za 78:5; Yos 1:8; Kum 33:4; 2Fal 22:8; Rum 3:2; 9:4Amemfunulia Yakobo neno lake,
sheria zake na maagizo yake kwa Israeli.
147:20 Rum 3:1-2; Kum 4:7-8, 32-34; Za 79:6; 103:1; 33:2; Mdo 14:16Hajafanya hivyo kwa taifa lingine lolote,
hawazijui sheria zake.
Msifuni Bwana.