Zaburi 147:1-11 NEN

Zaburi 147:1-11

Zaburi 147

Kumsifu Mungu Mwenye Nguvu Zote

147:1 Za 135:3; 33:1Msifuni Bwana.

Tazama jinsi ilivyo vyema kumwimbia Mungu wetu sifa,

jinsi inavyopendeza na kustahili kumsifu yeye!

147:2 Za 51:18; 106:47; Kum 30:3; Isa 27:13; Yer 32:37; Eze 36:24Bwana hujenga Yerusalemu,

huwakusanya Israeli walio uhamishoni.

147:3 Za 34:18; Isa 1:6; 61:1; Eze 34:16; Ebr 12:13; Ay 5:18; Lk 4:18Anawaponya waliovunjika mioyo

na kuvifunga vidonda vyao.

147:4 Mwa 15:5; Isa 40:26Huzihesabu nyota

na huipa kila moja jina lake.

147:5 Kut 14:31; Nah 1:3; 1Nya 16:25; Za 48:1; 145:3; Isa 40:28Bwana wetu ni mkuu na mwenye uwezo mwingi,

ufahamu wake hauna kikomo.

147:6 2Nya 33:23; Za 146:8, 9; 37:9, 10; 145:20Bwana huwahifadhi wanyenyekevu

lakini huwashusha waovu mpaka mavumbini.

147:7 Za 30:4; 33:3; 42:4; 27:6; 98:5; Efe 2:20Mwimbieni Bwana kwa shukrani,

mpigieni Mungu wetu kinubi.

147:8 Kum 32:2; 11:14; 2Sam 1:21; Ay 26:8; 38:26; 5:10; 28:26; Za 104:14Yeye huzifunika anga kwa mawingu,

huinyeshea ardhi mvua,

na kuzifanya nyasi kuota juu ya vilima.

147:9 Ay 38:41; Mt 6:26; Mwa 8:7; 1:30; Lk 12:24; Za 104:27, 28Huwapa chakula mifugo

na pia makinda ya kunguru yanapolia.

147:10 1Sam 16:7; Hos 1:7; Ay 39:11; Za 33:16-17Furaha yake haipo katika nguvu za farasi,

wala furaha yake kwenye miguu ya mwanadamu.

147:11 Za 35:27; 33:18; 103:11; 119:43; 6:4Bwana hupendezwa na wale wamchao,

wale wanaoweka tumaini lao katika upendo wake usiokoma.

Read More of Zaburi 147