Zaburi 144:9-15
144:9 Za 28:7; 96:1; 33:2-3; 71:22; 69:1Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya,
kwa zeze yenye nyuzi kumi nitakuimbia,
144:10 2Sam 8:14; Za 18:50; Ay 5:20kwa Yule awapaye wafalme ushindi,
ambaye humwokoa Daudi, mtumishi wake kutokana na upanga hatari.
144:11 Za 3:7; 25:20; 18:44; 41:6-7; 12:2; 36:3; 106:26; Isa 44:20Nikomboe na uniokoe
kutoka mikononi mwa wageni
ambao vinywa vyao vimejaa uongo,
na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.
144:12 Za 92:12-14; 128:3; 4:4; 7:4Kisha wana wetu wakati wa ujana wao
watakuwa kama mimea iliyotunzwa vizuri,
binti zetu watakuwa kama nguzo zilizoviringwa
kurembesha jumba la kifalme.
144:13 Mit 3:10Ghala zetu zitajazwa
aina zote za mahitaji.
Kondoo zetu watazaa kwa maelfu,
kwa makumi ya maelfu katika mashamba yetu;
144:14 Mit 14:4; 2Fal 25:11; Isa 24:11; Yer 14:2-3; Law 26:17maksai wetu watakokota
mizigo mizito.
Hakutakuwa na kubomoka kuta,
hakuna kuchukuliwa mateka,
wala kilio cha taabu
katika barabara zetu.
144:15 Kum 28:3; 33:29Heri watu ambao hili ni kweli;
heri wale ambao Bwana ni Mungu wao.