Zaburi 144:9-15 NEN

Zaburi 144:9-15

144:9 Za 28:7; 96:1; 33:2-3; 71:22; 69:1Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya,

kwa zeze yenye nyuzi kumi nitakuimbia,

144:10 2Sam 8:14; Za 18:50; Ay 5:20kwa Yule awapaye wafalme ushindi,

ambaye humwokoa Daudi, mtumishi wake kutokana na upanga hatari.

144:11 Za 3:7; 25:20; 18:44; 41:6-7; 12:2; 36:3; 106:26; Isa 44:20Nikomboe na uniokoe

kutoka mikononi mwa wageni

ambao vinywa vyao vimejaa uongo,

na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.

144:12 Za 92:12-14; 128:3; 4:4; 7:4Kisha wana wetu wakati wa ujana wao

watakuwa kama mimea iliyotunzwa vizuri,

binti zetu watakuwa kama nguzo zilizoviringwa

kurembesha jumba la kifalme.

144:13 Mit 3:10Ghala zetu zitajazwa

aina zote za mahitaji.

Kondoo zetu watazaa kwa maelfu,

kwa makumi ya maelfu katika mashamba yetu;

144:14 Mit 14:4; 2Fal 25:11; Isa 24:11; Yer 14:2-3; Law 26:17maksai wetu watakokota

mizigo mizito.

Hakutakuwa na kubomoka kuta,

hakuna kuchukuliwa mateka,

wala kilio cha taabu

katika barabara zetu.

144:15 Kum 28:3; 33:29Heri watu ambao hili ni kweli;

heri wale ambao Bwana ni Mungu wao.

Read More of Zaburi 144