Zaburi 140:6-13
140:6 Za 16:2; 28:2, 6Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.”
Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu,
unikingaye kichwa changu siku ya vita:
140:8 Za 10:2-3; 66:7; Ay 5:12-13Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao,
usiache mipango yao ikafanikiwa,
wasije wakajisifu.
140:9 Mit 18:7Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe
na shida zinazosababishwa na midomo yao.
140:10 Za 11:6; 21:9; Mt 3:10; Lk 12:40; Ufu 20:15Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie!
Na watupwe motoni,
katika mashimo ya matope,
wasiinuke tena kamwe.
140:11 Za 34:21Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi;
maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
140:12 1Fal 8:45; Za 35:10; 82:3; 109:31Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki,
na kuitegemeza njia ya mhitaji.
140:13 Za 138:2; 11:7; 16:11Hakika wenye haki watalisifu jina lako,
na waadilifu wataishi mbele zako.