Zaburi 140:1-5
Zaburi 140
Kuomba Ulinzi Wa Mungu
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
140:1 Za 17:13; 25:20; 59:2; 71:4; 142:6; 143:9; 86:14Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu;
nilinde na watu wenye jeuri,
140:2 Mit 6:14; 16:27; Isa 59:4; Hos 7:15; Za 36:4; 52:2; 68:30ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao,
na kuchochea vita siku zote.
140:3 Za 57:4; 58:4; Rum 3:13; Yak 3:8Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka,
sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
140:4 Za 141:9; 36:11Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu;
nilinde na watu wenye jeuri
wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
140:5 Ay 34:30; Za 31:4; 38:12; 119:110; Ay 18:8; 18:9Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa,
wametandaza kamba za wavu wao,
wametega mitego kwenye njia yangu.