Zaburi 139:17-24
139:17 Za 92:5; Ay 5:9Tazama jinsi yalivyo ya thamani mawazo yako kwangu, Ee Mungu!
Jinsi jumla yake ilivyo kubwa!
139:18 Za 40:5; 3:5; Ay 29:18Kama ningezihesabu,
zingekuwa nyingi kuliko mchanga.
Niamkapo,
bado niko pamoja nawe.
139:19 Za 5:6; 6:8; 59:2; Isa 11:4Laiti ungewachinja waovu, Ee Mungu!
Ondokeni kwangu, ninyi wamwaga damu!
139:20 Za 65:7; Kum 5:11; Ay 21:14-15; Yud 15Wanazungumza juu yako wakiwa na kusudi baya,
adui zako wanatumia vibaya jina lako.
139:21 2Nya 19:2; Za 31:6; 26:5; 119:113Ee Bwana, je, nisiwachukie wanaokuchukia?
Nisiwachukie sana wanaoinuka dhidi yako?
139:22 Mt 5:43Sina kitu zaidi ya chuki dhidi yao,
ninawahesabu ni adui zangu.
139:23 Ay 31:6; 1Sam 16:7; 1Nya 29:17; Za 7:9; Mit 17:3; Yer 11:20; Ufu 2:23Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu,
nijaribu na ujue mawazo yangu.
139:24 Yer 25:5; 36:3; Za 5:8; 23:2; 143:10Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu,
uniongoze katika njia ya milele.