Zaburi 139:11-16
Kama nikisema, “Hakika giza litanificha
na nuru inayonizunguka iwe usiku,”
139:12 Ay 34:22; Dan 2:22hata giza halitakuwa giza kwako,
usiku utangʼaa kama mchana,
kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.
139:13 Za 119:73; Ay 10:11; Isa 44:2, 24; 46:3; 49:5; Yer 1:5Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani;
uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.
Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa
kwa namna ya ajabu na ya kutisha;
kazi zako ni za ajabu,
ninajua hayo kikamilifu.
139:15 Mhu 11:5; Ay 10:11; Za 63:9Umbile langu halikufichika kwako,
nilipoumbwa mahali pa siri.
Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,
139:16 Ay 33:29; Za 90:12macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika.
Siku zangu zote ulizonipangia
ziliandikwa katika kitabu chako
kabla haijakuwepo hata moja.