Zaburi 136:13-26
136:13 Za 78:13Kwake yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu,
Fadhili zake zadumu milele.
136:14 Kut 14:22; Za 106:9Na kuwapitisha Israeli katikati yake,
Fadhili zake zadumu milele.
136:15 Kut 14:27Lakini alimfagia Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu,
Fadhili zake zadumu milele.
136:16 Kut 13:18; Za 78:52Kwake yeye aliyewaongoza watu wake katika jangwa,
Fadhili zake zadumu milele.
136:17 Hes 21:23-25; Yos 24:8-11; Za 78:55; 135:9-12Ambaye aliwapiga wafalme wenye nguvu,
Fadhili zake zadumu milele.
136:18 Kum 29:7; Yos 12:7-24Naye aliwaua wafalme wenye nguvu,
Fadhili zake zadumu milele.
136:19 Hes 21:21-25Sihoni mfalme wa Waamori,
Fadhili zake zadumu milele.
136:20 Hes 21:33-35Ogu mfalme wa Bashani,
Fadhili zake zadumu milele.
136:21 Kum 1:38; Yos 12:1; 14:1Akatoa nchi yao kuwa urithi,
Fadhili zake zadumu milele.
136:22 Kum 29:8; Za 78:55; Isa 20:3; 41:8; 42:19; 43:10; 44:1, 21; 45:4; 49:5-7Urithi kwa Israeli mtumishi wake,
Fadhili zake zadumu milele.
136:23 Za 78:29; 103:14; 115:12Aliyetukumbuka katika unyonge wetu,
Fadhili zake zadumu milele.
136:24 Yos 10:14; Neh 9:28; Kum 6:19Alituweka huru toka adui zetu,
Fadhili zake zadumu milele.
136:25 Mwa 1:30; Mit 6:26Ambaye humpa chakula kila kiumbe.
Fadhili zake zadumu milele.
136:26 Za 105:1; 115:3; Ezr 3:11Mshukuruni Mungu wa mbinguni,
Fadhili zake zadumu milele.