Zaburi 135:13-21
135:13 Kut 3:15; Za 102:12Ee Bwana, jina lako ladumu milele,
kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
135:14 1Sam 24:15; Ebr 10:30; Kum 32:36Maana Bwana atawathibitisha watu wake,
na kuwahurumia watumishi wake.
135:15 Ufu 9:20; Isa 2:8; 31:7; 37:19; 40:19; Yer 1:16; 10:5; Za 96:5Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu,
zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
135:16 1Fal 18:26Zina vinywa, lakini haziwezi kusema,
zina macho, lakini haziwezi kuona;
135:17 Yer 10:14; Hab 2:19zina masikio, lakini haziwezi kusikia,
wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo,
vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
135:19 Za 22:23Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana;
ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana;
ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
135:21 Za 128:5; 134:3; 1Fal 8:13; 2Nya 6:2Msifuni Bwana kutoka Sayuni,
msifuni yeye aishiye Yerusalemu.
Msifuni Bwana.