Zaburi 127:1-5 NEN

Zaburi 127:1-5

Zaburi 127

Bila Mungu, Kazi Ya Mwanadamu Haifai

Wimbo wa kwenda juu. Wa Solomoni.

127:1 Za 78:69; 121:4Bwana asipoijenga nyumba,

wajengao hufanya kazi bure.

Bwana asipoulinda mji,

walinzi wakesha bure.

127:2 Mwa 3:17; Hes 6:26; Ay 11:18; Kum 33:12; Mhu 2:25Mnajisumbua bure kuamka mapema

na kuchelewa kulala,

mkitaabikia chakula:

kwa maana yeye huwapa usingizi wapenzi wake.

127:3 Mwa 1:28; 33:5; Kum 28:4Wana ni urithi utokao kwa Bwana,

watoto ni zawadi kutoka kwake.

127:4 Za 112:2Kama mishale mikononi mwa shujaa

ndivyo walivyo wana awazaao mtu katika ujana wake.

127:5 Za 128:2-3; Mwa 24:60; 23:10Heri mtu ambaye podo lake

limejazwa nao.

Hawataaibishwa wanaposhindana

na adui zao langoni.

Read More of Zaburi 127