Zaburi 120:1-7
Zaburi 120
Kuomba Msaada
Wimbo wa kwenda juu.
120:1 2Sam 22:7; Za 18:1; 118:5Katika dhiki yangu namwita Bwana,
naye hunijibu.
120:2 Za 31:18; 52:4Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo
na ndimi za udanganyifu.
Atakufanyia nini,
au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
120:4 Kum 32:23Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa,
kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
120:5 Mwa 25:13; 2:10; Yer 2:10; 49:28; 1Sam 25:1Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki,
kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Nimeishi muda mrefu mno
miongoni mwa wale wanaochukia amani.
Mimi ni mtu wa amani;
lakini ninaposema, wao wanataka vita.