Zaburi 119:89-96
Imani Katika Sheria Ya Bwana
119:89 Za 119:111, 144; 111:8; Isa 51:6; Mt 5:18; 1Pet 1:25Ee Bwana, neno lako ni la milele,
linasimama imara mbinguni.
119:90 Za 36:5; 45:17; 148:6; Ay 8:19Uaminifu wako unaendelea kwa vizazi vyote,
umeiumba dunia, nayo inadumu.
119:91 Yer 33:25; 31:35; Za 148:6; 104:2-4; Mwa 8:22Sheria zako zinadumu hadi leo,
kwa kuwa vitu vyote vinakutumikia.
119:92 Za 37:4, 5; 112:1; 119:50, 67; Rum 15:4Kama nisingefurahia sheria yako,
ningeangamia katika taabu zangu.
119:93 Za 119:83; 103:5Sitasahau mausia yako kamwe,
kwa maana kwayo umehifadhi maisha yangu.
119:94 Za 119:45, 146; 54:1; 116:4; Yer 17:14; 31:18; 42:11; Hos 2:7, 16Uniokoe, kwa maana mimi ni wako,
kwa kuwa nimetafuta mausia yako.
119:95 Za 69:4; 119:99Waovu wanangojea kuniangamiza,
bali mimi ninatafakari sheria zako.
119:96 Za 19:7; Isa 40:8; Mt 5:18Katika ukamilifu wote ninaona mna kikomo,
lakini amri zako hazina mpaka.