Zaburi 119:73-80
Haki Ya Sheria Ya Bwana
119:73 Mwa 1:27; Ay 4:17; 10:8; Za 139:13-16; 100:3; 138:8Mikono yako ilinifanya na kuniumba,
nipe ufahamu niweze kujifunza amri zako.
119:74 Za 34:2; 119:9; 130:5Wakuchao wafurahie wanaponiona,
kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika neno lako.
119:75 Za 89:30, 31; 119:7, 138, 172; Ebr 12:5-11Ee Bwana, ninajua kwamba sheria zako ni za haki,
katika uaminifu wako umeniadhibu.
119:76 Za 6:4; 119:41Upendo wako usiokoma uwe faraja yangu,
sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.
Huruma yako na inijie ili nipate kuishi,
kwa kuwa naifurahia sheria yako.
119:78 Za 119:51; 35:19; 119:86, 161; 25:3; Yer 50:32Wenye majivuno na waaibishwe kwa kunikosea mimi bila sababu,
lakini mimi nitatafakari juu ya mausia yako.
119:79 Za 119:27, 125Wale wakuchao na wanigeukie mimi,
hao ambao wanazielewa sheria zako.
119:80 Za 119:1; 119:6; 1Fal 8:61; Mwa 26:5Moyo wangu usiwe na lawama katika kutii maagizo yako,
ili nisiaibishwe.