Zaburi 119:57-64
Kujitolea Katika Sheria Ya Bwana
119:57 Kum 32:9; Yer 51:19; Za 119:17, 67, 101; Mao 3:24Ee Bwana, wewe ni fungu langu,
nimeahidi kuyatii maneno yako.
119:58 Kum 4:29; Ezr 9:8; 1Nya 16:11; Za 34:4; 119:41; Mwa 43:29Nimetafuta uso wako kwa moyo wangu wote,
nihurumie sawasawa na ahadi yako.
119:59 Yoe 2:13; Lk 15:17; Yos 24:14, 15Nimezifikiri njia zangu
na nimeelekeza hatua zangu katika mausia yako.
119:60 Za 119:115Nitafanya haraka bila kuchelewa
kuzitii amri zako.
119:61 Za 119:83, 109, 153, 176Hata waovu wanifunge kwa kamba,
sitasahau sheria yako.
119:62 Za 119:55; 119:7; Mdo 16:25Usiku wa manane ninaamka kukushukuru
kwa sababu ya sheria zako za haki.
119:63 Za 15:4; 101:6, 7; 103:11; 119:56; 111:10Mimi ni rafiki kwa wale wote wakuchao,
kwa wote wanaofuata mausia yako.
119:64 Za 33:5; 119:12, 108Ee Bwana, dunia imejaa upendo wako,
nifundishe maagizo yako.