Zaburi 119:49-56
Matumaini Katika Sheria Ya Bwana
119:49 Za 119:9, 43Kumbuka neno lako kwa mtumishi wako,
kwa sababu umenipa tumaini.
119:50 Za 119:25; 27:13; Yer 15:16; Rum 5:3-5; Ebr 6:17-19Faraja yangu katika mateso yangu ni hii:
Ahadi yako inahifadhi maisha yangu.
119:51 Za 119:21; Ay 16:10; 17:2; 23:11; Yer 20:7Wenye majivuno wamenisimanga bila kuchoka,
hata hivyo sitaiacha sheria yako.
119:52 Za 103:18Ee Bwana, ninazikumbuka sheria zako za zamani,
nazo zinanifariji.
119:53 Kut 32:19; 33:4; Za 89:30; Ezr 9:3Nimeshikwa sana na ghadhabu kwa ajili ya waovu,
ambao wameacha sheria yako.
119:54 Za 119:172; 101:1; 138:5Maagizo yako ni kiini cha nyimbo zangu
popote ninapoishi.
119:55 Za 119:44, 62, 72; 1:2; 42:8; 63:6; 77:2; Isa 26:9; Mdo 16:25Ee Bwana, wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako,
nami nitatii sheria yako.
119:56 Za 119:4, 100, 134; Hes 15:40Hili limekuwa zoezi langu:
nami ninayatii mausia yako.