Zaburi 119:33-40
Maombi Ili Kupata Ufahamu Wa Sheria
119:33 Za 119:12Ee Bwana, nifundishe kuyafuata maagizo yako,
nami nitayashika mpaka mwisho.
119:34 Za 119:27, 69, 73, 144, 169; Mit 2:6; Ay 32:8; Yak 1:5; Kum 6:25; Dan 2:21Nipe ufahamu, nami nitaishika sheria yako
na kuitii kwa moyo wangu wote.
119:35 Za 119:32; 1:2; 25:4, 5Niongoze kwenye njia ya amri zako,
kwa kuwa huko napata furaha.
119:36 Yos 24:23; Ebr 13:5; Mk 7:21; 12:15; Eze 33:31; 1Tim 6:10Ugeuze moyo wangu kuelekea sheria zako,
na siyo kwenye mambo ya ubinafsi.
119:37 Za 119:9, 25; 71:20; Ay 31:1Geuza macho yangu kutoka kwenye mambo yasiyofaa,
uyahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
119:38 Hes 23:19; 2Sam 7:25Mtimizie mtumishi wako ahadi yako,
ili upate kuogopwa.
119:39 Za 119:22; 69:9; 89:51; Isa 25:8; 51:7; 54:4Niondolee aibu ninayoiogopa,
kwa kuwa sheria zako ni njema.
119:40 Za 119:20, 25, 149, 154Tazama jinsi ninavyoonea shauku mausia yako!
Hifadhi maisha yangu katika haki yako.