Zaburi 119:25-32
Kuamua Kuitii Sheria Ya Bwana
119:25 Za 44:25; 143:11; 119:9, 50, 107Nimelazwa chini mavumbini,
yahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
119:26 Za 25:4; 27:11; 86:11; 1Fal 8:36Nilikueleza njia zangu ukanijibu,
nifundishe sheria zako.
119:27 Za 105:2; 145:5Nijulishe mafundisho ya mausia yako,
nami nitatafakari maajabu yako.
119:28 Za 119:9; 116:3; 18:1; 6:7; Yer 45:3; Isa 51:11; 40:29; 41:10Nafsi yangu imechakazwa kwa huzuni,
uniimarishe sawasawa na neno lako.
119:29 Za 26:4; Hes 6:25; Mit 30:8; Ebr 8:10Niepushe na njia za udanganyifu,
kwa neema unifundishe sheria zako.
119:30 Yos 24:22; Za 26:3; 108:1Nimechagua njia ya kweli,
nimekaza moyo wangu katika sheria zako.
119:31 Kum 10:20Nimengʼangʼania sheria zako, Ee Bwana,
usiniache niaibishwe.
119:32 1Fal 4:29; Isa 60:5; 2Kor 6:11Nakimbilia katika njia ya maagizo yako,
kwa kuwa umeuweka moyo wangu huru.