Zaburi 119:17-24
Furaha Katika Sheria Ya Bwana
119:17 Za 13:6; 116:7; 119:67; 103:20Mtendee mema mtumishi wako, nami nitaishi;
nitalitii neno lako.
Yafungue macho yangu nipate kuona
mambo ya ajabu katika sheria yako.
119:19 Mwa 23:4; Ebr 11:13Mimi ni mgeni duniani,
usinifiche amri zako.
119:20 Za 84:2; 119:131; 42:2; 63:1; Isa 26:9Nafsi yangu inataabika kwa shauku kubwa
juu ya sheria zako wakati wote.
119:21 Za 119:10, 51; 5:5; Ay 30:1; Yer 20:7; 50:32; Kum 27:26; Dan 4:37; Mal 3:15Unawakemea wenye majivuno, waliolaaniwa
waendao mbali na amri zako.
119:22 Za 39:8; 119:2Niondolee dharau na dhihaka,
kwa kuwa ninazishika sheria zako.
Ingawa watawala huketi pamoja na kunisingizia,
mtumishi wako atatafakari juu ya maagizo yako.
Sheria zako ni furaha yangu,
nazo ni washauri wangu.