Zaburi 119:161-168
Kujiweka Wakfu Kwa Sheria Ya Bwana
119:161 Za 119:23, 122, 157; 119:120; 1Sam 24:14-15Watawala wamenitesa bila sababu,
lakini moyo wangu unatetemeka kwa neno lako.
119:162 Za 119:25; 41:2Nafurahia ahadi zako
kama mtu aliyepata mateka mengi.
Ninachukia na kuchukizwa sana na uongo,
lakini napenda sheria yako.
119:164 Za 119:111; 1Sam 30:16; Isa 9:3; 53:12Ninakusifu mara saba kwa siku,
kwa ajili ya sheria zako za haki.
119:165 Za 119:11; 37:11; 37:24; Isa 26:3, 12; 27:5; 32:17; 57:19; 66:12; 1Yn 2:10; Mit 3:2Wanaopenda sheria yako wana amani tele,
wala hakuna kitu kinachoweza kuwakwaza.
119:166 Za 119:81Ee Bwana, ninangojea wokovu wako,
nami ninafuata amri zako,
119:167 Za 119:47Ninazitii sheria zako,
kwa sababu ninazipenda mno.
119:168 Za 139:3; Ay 10:4; 23:10; Mit 5:21Nimetii mausia yako na sheria zako,
kwa kuwa njia zangu zote zinajulikana kwako.