Zaburi 119:153-160
Maombi Kwa Ajili Ya Msaada
119:153 Za 13:3; 3:7; 44:17; Mao 5:1Yaangalie mateso yangu, uniokoe,
kwa kuwa sijasahau sheria yako.
119:154 Za 119:24, 41; 35:1; 1Sam 24:15; Yer 50:34; Mik 7:9Nitetee katika hali hii yangu na unikomboe,
uyahifadhi maisha yangu sawasawa na ahadi yako.
119:155 Za 119:94, 118; Ay 5:4Wokovu uko mbali na waovu,
kwa kuwa hawatafuti maagizo yako.
119:156 Neh 9:27; Yak 5:11; Za 119:25, 149Ee Bwana, huruma zako ni kuu,
uyahifadhi maisha yangu sawasawa na sheria zako.
119:157 Za 7:1; 44:18Adui wanaonitesa ni wengi,
lakini mimi sitaziacha sheria zako.
119:158 Za 119:104, 136; Kut 32:19Ninawatazama wasioamini kwa chuki,
kwa kuwa hawalitii neno lako.
119:159 Za 119:25; 41:2Tazama jinsi ninavyopenda mausia yako;
Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na upendo wako.
119:160 Za 119:89; 111:8Maneno yako yote ni kweli,
sheria zako zote za haki ni za milele.