Zaburi 119:129-136
Shauku Ya Kuitii Sheria Ya Bwana
119:129 Za 119:18, 22, 88Sheria zako ni za ajabu,
hivyo ninazitii.
119:130 Za 119:105; 19:7, 10; Mit 1:4; 2Pet 1:19Kuingia kwa maneno yako kunaleta nuru,
kunampa mjinga ufahamu.
119:131 Za 42:1; 119:20Nimefungua kinywa changu na kuhema,
nikitamani amri zako.
119:132 2Sam 24:14; Kut 4:31; Za 6:4; 9:13; 5:11; 106:4; 1Sam 1:11Nigeukie na unihurumie, kama uwafanyiavyo siku zote
wale wanaolipenda jina lako.
119:133 Kum 6:12; Za 119:9, 11, 122; Rum 6:16Ongoza hatua zangu kulingana na neno lako,
usiache dhambi yoyote initawale.
119:134 Lk 1:74; Za 119:56, 88, 122Niokoe na uonevu wa wanadamu,
ili niweze kutii mausia yako.
119:135 Hes 6:25; Za 4:6; 80:3; 4:6; 119:12Mwangazie mtumishi wako uso wako
na unifundishe amri zako.
119:136 Yer 9:1; 9:1, 18; 13:17; 14:17; Mao 1:16; 3:48; Isa 22:4; 42:24; Eze 9:4; Za 6:6; 119:158; 106:25Chemchemi za machozi zinatiririka kutoka machoni yangu,
kwa kuwa sheria yako haifuatwi.