Zaburi 118:1-16
Zaburi 118
Shukrani Kwa Ajili Ya Ushindi
118:1 1Nya 16:8; Ezr 3:11; 2Nya 7:3; 5:13Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema;
upendo wake wadumu milele.
118:2 Za 115:9; 106:1; 136:1-26Israeli na aseme sasa:
“Upendo wake wadumu milele.”
118:3 Kut 30:30; Za 115:10Nyumba ya Aroni na iseme sasa:
“Upendo wake wadumu milele.”
118:4 Za 115:11Wote wamchao Bwana na waseme sasa:
“Upendo wake wadumu milele.”
118:5 Za 18:6; 31:7; 77:2; 120:1; 118:21; 34:4; 86:7; 116:1; 138:3Wakati wa maumivu yangu makuu nilimlilia Bwana,
naye akanijibu kwa kuniweka huru.
118:6 Kum 31:6; Ebr 13:5; Za 56:5Bwana yuko pamoja nami, sitaogopa.
Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
118:7 Kum 33:29; Ebr 13:6; Za 54:4Bwana yuko pamoja nami,
yeye ni msaidizi wangu.
Nitawatazama adui zangu
wakiwa wameshindwa.
118:8 Yer 17:5, 7; Za 9:9; 62:8; 5:11; 37:3; 40:4; 108:12; Isa 25:4; 57:13; 2:22; 2Nya 32:7-8Ni bora kumkimbilia Bwana
kuliko kumtumainia mwanadamu.
118:9 Za 146:3; Isa 30:2, 3Ni bora kumkimbilia Bwana
kuliko kuwatumainia wakuu.
118:10 Za 37:9Mataifa yote yalinizunguka,
lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
118:11 Za 88:17; 3:6Walinizunguka pande zote,
lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
118:12 Mhu 7:6; Za 58:9; 37:9; Kum 1:44Walinizunguka kama kundi la nyuki,
lakini walikufa haraka kama miiba iteketeayo;
kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
118:13 Za 118:7; 86:17; 2Nya 18:31Nilisukumwa nyuma karibu kuanguka,
lakini Bwana alinisaidia.
118:14 Kut 15:2; Za 62:2Bwana ni nguvu yangu na wimbo wangu,
yeye amefanyika wokovu wangu.
118:15 Ay 8:21; Lk 1:51; Za 106:5; 89:13; 108:6; Kut 15:6Sauti za shangwe na ushindi
zinavuma hemani mwa wenye haki:
“Mkono wa kuume wa Bwana
umetenda mambo makuu!
118:16 Kut 15:6Mkono wa kuume wa Bwana
umeinuliwa juu,
mkono wa kuume wa Bwana
umetenda mambo makuu!”