Zaburi 116:12-19
116:12 Za 103:2; 106:1Nimrudishie Bwana nini
kwa wema wake wote alionitendea?
116:13 Za 105:1Nitakiinua kikombe cha wokovu
na kulitangaza jina la Bwana.
116:14 Hes 30:2; Za 66:13Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana
mbele za watu wake wote.
116:15 Za 72:14; Hes 23:10; Ay 5:26; Lk 16:22; Ufu 14:13Kifo cha watakatifu kina thamani
machoni pa Bwana.
116:16 Za 119:125; 143:12; 86:16; Ay 12:18Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako,
mimi ni mtumishi wako,
mwana wa mjakazi wako;116:16 Au: mwanao mwaminifu.
umeniweka huru
toka katika minyororo yangu.
116:17 Law 7:12; Ezr 1:4Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru
na kuliita jina la Bwana.
116:18 Za 116:14; Law 22:18Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana
mbele za watu wake wote,
116:19 Za 102:21; 92:13; 135:2; 96:8; 100:4katika nyua za nyumba ya Bwana,
katikati yako, ee Yerusalemu.
Msifuni Bwana.