Zaburi 116:1-11
Zaburi 116
Shukrani Kwa Kuokolewa Kutoka Mauti
116:1 Za 18:1; 31:22; 40:1; 6:9; 28:2Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu;
amesikia kilio changu ili anihurumie.
116:2 Za 5:1Kwa sababu amenitegea sikio lake,
nitamwita siku zote za maisha yangu.
116:3 2Sam 22:6; Za 18:4-5Kamba za mauti zilinizunguka,
maumivu makuu ya kuzimu yalinipata,
nikalemewa na taabu na huzuni.
116:4 Za 80:2, 18; 118:5Ndipo nikaliitia jina la Bwana:
“Ee Bwana, niokoe!”
116:5 Kut 22:27; 9:27; Ezr 9:15; Za 11:7; 86:15; 2Nya 12:6; Neh 9:8; Yer 12:1; Mao 1:18; Ufu 16:5Bwana ni mwenye neema na haki,
Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
116:6 Za 79:8; 18:3; 22:5; 107:13Bwana huwalinda wanyenyekevu,
nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
116:7 Za 13:6; 106:1; 142:7; 46:10; 62:1; 131:2; Mt 11:29; Yer 6:16Ee nafsi yangu, tulia tena,
kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
116:8 Za 86:13Kwa kuwa wewe, Ee Bwana,
umeniokoa nafsi yangu na mauti,
macho yangu kutokana na machozi,
miguu yangu kutokana na kujikwaa,
116:9 Mwa 5:22; Za 56:13; 89:15; 27:13; Ay 28:13; Isa 38:11; Yer 11:9ili niweze kutembea mbele za Bwana,
katika nchi ya walio hai.
116:10 Za 9:18; 72:2; 107:17; 119:67, 71, 75; 2Kor 4:13Niliamini, kwa hiyo nilisema,
“Mimi nimeteseka sana.”
116:11 Yer 9:3-5Katika taabu yangu nilisema,
“Wanadamu wote ni waongo.”