Zaburi 115:1-11 NEN

Zaburi 115:1-11

Zaburi 115

Mungu Mmoja Wa Kweli

115:1 Za 29:2; 96:8; Kut 34:6Sio kwetu sisi, Ee Bwana, sio kwetu sisi,

bali utukufu ni kwa jina lako,

kwa sababu ya upendo

na uaminifu wako.

115:2 Za 42:3, 10; 79:10; Yoe 2:17Kwa nini mataifa waseme,

“Yuko wapi Mungu wao?”

115:3 Ezr 5:11; Neh 1:4; Za 136:26; 135:6; 103:19; Mit 6:9; Dan 4:35; 1Nya 16:26Mungu wetu yuko mbinguni,

naye hufanya lolote limpendezalo.

115:4 2Fal 19:18; 2Nya 32:19; Yer 10:3-5; Mdo 19:26; Kum 4:28; Ufu 9:20; Za 135:15, 16; Isa 40:19; Hos 8:6; 1Kor 10:19, 20Lakini sanamu zao ni za fedha na dhahabu,

zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.

115:5 Yer 10:5Zina vinywa, lakini haziwezi kusema,

zina macho, lakini haziwezi kuona;

zina masikio, lakini haziwezi kusikia,

zina pua, lakini haziwezi kunusa;

zina mikono, lakini haziwezi kupapasa,

zina miguu, lakini haziwezi kutembea;

wala koo zao haziwezi kutoa sauti.

115:8 Za 135:18; Isa 44:9, 10; Yon 2:8; Hab 2:18Wale wanaozitengeneza watafanana nazo,

vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.

115:9 Za 37:3; 62:8; 33:20; Mit 30:5Ee nyumba ya Israeli, mtumainini Bwana,

yeye ni msaada na ngao yao.

115:10 Kut 30:30; Za 118:3; Mal 2:7Ee nyumba ya Aroni, mtumainini Bwana,

yeye ni msaada na ngao yao.

115:11 Za 22:23; 103:11; 118:4Ninyi mnaomcha, mtumainini Bwana,

yeye ni msaada na ngao yao.

Read More of Zaburi 115