Zaburi 109:21-31
109:21 Kut 9:16; Za 3:7; 23:3; 69:16Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi,
unitendee wema kwa ajili ya jina lako,
uniokoe kwa wema wa pendo lako.
Maana mimi ni maskini na mhitaji,
moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
109:23 Ay 14:2Ninafifia kama kivuli cha jioni,
nimerushwa-rushwa kama nzige.
109:24 Ebr 12:12; Ay 16:8; Za 35:13Magoti yangu yamelegea kwa kufunga,
mwili wangu umedhoofika na kukonda.
109:25 Za 22:6; Ay 16:4; Mt 27:39; Mk 15:29; Isa 37:22Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu,
wanionapo, hutikisa vichwa vyao.
109:26 Za 12:1; 119:86Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie,
niokoe sawasawa na upendo wako.
109:27 Ay 37:7Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako,
kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.
109:28 2Sam 16:12; Za 66:4; Isa 35:10; 51:11; 54:1; 65:14; Hes 22:12Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki,
watakaposhambulia wataaibishwa,
lakini mtumishi wako atashangilia.
109:29 Za 35:26Washtaki wangu watavikwa fedheha,
na kufunikwa na aibu kama joho.
109:30 Za 35:18Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana,
katika umati mkubwa nitamsifu.
109:31 Za 16:8; 108:6Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji,
kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.