Zaburi 109:1-20
Zaburi 109
Lalamiko La Mtu Aliyeko Kwenye Shida
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
109:1 Kut 15:2; Yer 17:14; Ay 34:29; Za 83:1Ee Mungu, ambaye ninakusifu,
usiwe kimya,
109:2 Za 43:1; 52:4kwa maana watu waovu na wadanganyifu
wamefungua vinywa vyao dhidi yangu;
wasema dhidi yangu
kwa ndimi za udanganyifu.
109:3 Za 69:4; 35:7; 35:7, 10; Yn 15:25; 1Sam 19:4, 5Wamenizunguka kwa maneno ya chuki,
wananishambulia bila sababu.
109:4 Za 69:13; 141:5Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki,
lakini mimi ninawaombea.
109:5 Mwa 44:4; Za 38:20Wananilipiza mabaya kwa mema,
chuki badala ya urafiki wangu.
109:6 1Nya 21:1; Ay 1:6; Zek 3:1Agiza mtu mwovu ampinge,
mshtaki109:6 Mshtaki hapa maana yake ni Shetani. asimame mkono wake wa kuume.
109:7 Za 1:5; Mit 28:9; Zek 3:1Anapohukumiwa, apatikane na hatia,
nayo maombi yake yamhukumu.
109:8 Ay 15:32; Mdo 1:20Siku zake za kuishi na ziwe chache,
nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.
109:9 Kut 22:24; Yer 18:21Watoto wake na waachwe yatima,
mke wake na awe mjane.
109:10 Mwa 4:12Watoto wake na watangetange wakiomba,
na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.
109:11 Hes 14:3; Isa 1:7; 6:11; 36:1; Mao 5:2; Neh 5:3; Ay 20:18; 18:9Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo,
matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.
109:12 Ay 5:4Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema
wala wa kuwahurumia yatima wake.
109:13 Za 21:10; 9:5; 37:28; Hes 14:12; Mit 10:7; Ay 18:19Uzao wake na ukatiliwe mbali,
majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.
109:14 Kut 20:5Maovu ya baba zake na yakumbukwe
mbele za Bwana,
dhambi ya mama yake
isifutwe kamwe.
109:15 Za 90:8; Kut 17:14; Kum 32:26; Ay 18:17Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana,
ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.
109:16 Ay 20:19; Za 35:10; 34:18Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema,
bali alimfukuza mnyonge na mhitaji,
aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.
109:17 Mit 28:27; Mt 7:2Alipenda kulaani,
nayo laana ikampata;
hakupenda kubariki,
kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.
109:18 Za 10:7; Hes 5:22Alivaa kulaani kama vazi lake,
nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji,
kwenye mifupa yake kama mafuta.
109:19 Za 109:29; 73:6; Eze 7:27Na iwe kama joho alilozungushiwa,
kama mshipi aliofungiwa daima.
109:20 Kut 32:34; Za 54:5; 94:23; 7:10; Isa 3:11; 2Tim 4:14Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu,
kwa wale wanaoninenea mabaya.