Zaburi 108:1-5
Zaburi 108
Kuomba Msaada Dhidi Ya Adui
(Zaburi 57:7-11; 60:5-12)
Wimbo. Zaburi ya Daudi.
108:1 Za 112:7; 119:30, 112; 18:49Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti;
nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
108:2 Ay 21:12Amka, kinubi na zeze!
Nitayaamsha mapambazuko.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa;
nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
108:4 Hes 14:18; Kum 7:9; Kut 34:6; Za 36:5; Mik 7:18-20Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu;
uaminifu wako unazifikia anga.
108:5 Za 8:1; 57:5Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,
utukufu wako na uenee duniani kote.