Zaburi 107:10-22 NEN

Zaburi 107:10-22

107:10 Za 107:14; 88:6; 143:3; 102:20; Isa 9:2; 42:7, 16; 49:9; 61:1; Mik 7:9; Ay 36:8Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu,

wafungwa wakiteseka katika minyororo,

107:11 Za 5:10; Hes 14:11; 1Fal 22:5; 2Nya 36:16kwa sababu walikuwa wameasi

dhidi ya maneno ya Mungu

na kudharau shauri

la Aliye Juu Sana.

107:12 Isa 63:5; Za 72:12; 2Fal 14:26Aliwatumikisha kwa kazi ngumu;

walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.

107:13 Za 106:8Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao,

naye akawaokoa kutoka taabu yao.

107:14 Isa 9:2; 42:7; 59:9; 50:10; 60:2; 29:18; Ay 36:8; Lk 1:79; Za 86:13; 116:16; 146:7; Mdo 12:7Akawatoa katika giza na huzuni kuu

na akavunja minyororo yao.

107:15 Za 107:8, 21, 31; 105:1; 6:4; 75:1Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma,

na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,

107:16 Isa 45:2kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba

na kukata mapingo ya chuma.

107:17 Za 53:1; 25:7; Law 14:1; 26:16; Isa 65:6, 7; Yer 30:14, 15; Gal 6:7, 8; Mt 1:22; Mao 3:39Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao,

wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.

107:18 Ay 3:24; 6:6; 17:16; 33:22Wakachukia kabisa vyakula vyote,

wakakaribia malango ya mauti.

107:19 Za 107:13; 5:2; 34:4Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao,

naye akawaokoa kutoka taabu yao.

107:20 Kum 32:2; Mt 8:8; 2Fal 20:4; Lk 7:7; Kut 15:26; Hes 21:8; Za 30:3; 16:10; 56:13; 147:15; Ay 33:28Akalituma neno lake na kuwaponya,

akawaokoa kutoka maangamizo yao.

107:21 Za 107:15; 6:4; 75:1Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma,

na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.

107:22 Law 7:12; Za 9:11; 73:28; 65:8; 50:14; 118:17; Ay 8:21; Ebr 13:15Na watoe dhabihu za kushukuru,

na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.

Read More of Zaburi 107