Zaburi 107:10-22
107:10 Za 107:14; 88:6; 143:3; 102:20; Isa 9:2; 42:7, 16; 49:9; 61:1; Mik 7:9; Ay 36:8Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu,
wafungwa wakiteseka katika minyororo,
107:11 Za 5:10; Hes 14:11; 1Fal 22:5; 2Nya 36:16kwa sababu walikuwa wameasi
dhidi ya maneno ya Mungu
na kudharau shauri
la Aliye Juu Sana.
107:12 Isa 63:5; Za 72:12; 2Fal 14:26Aliwatumikisha kwa kazi ngumu;
walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
107:13 Za 106:8Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao,
naye akawaokoa kutoka taabu yao.
107:14 Isa 9:2; 42:7; 59:9; 50:10; 60:2; 29:18; Ay 36:8; Lk 1:79; Za 86:13; 116:16; 146:7; Mdo 12:7Akawatoa katika giza na huzuni kuu
na akavunja minyororo yao.
107:15 Za 107:8, 21, 31; 105:1; 6:4; 75:1Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma,
na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
107:16 Isa 45:2kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba
na kukata mapingo ya chuma.
107:17 Za 53:1; 25:7; Law 14:1; 26:16; Isa 65:6, 7; Yer 30:14, 15; Gal 6:7, 8; Mt 1:22; Mao 3:39Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao,
wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
107:18 Ay 3:24; 6:6; 17:16; 33:22Wakachukia kabisa vyakula vyote,
wakakaribia malango ya mauti.
107:19 Za 107:13; 5:2; 34:4Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao,
naye akawaokoa kutoka taabu yao.
107:20 Kum 32:2; Mt 8:8; 2Fal 20:4; Lk 7:7; Kut 15:26; Hes 21:8; Za 30:3; 16:10; 56:13; 147:15; Ay 33:28Akalituma neno lake na kuwaponya,
akawaokoa kutoka maangamizo yao.
107:21 Za 107:15; 6:4; 75:1Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma,
na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
107:22 Law 7:12; Za 9:11; 73:28; 65:8; 50:14; 118:17; Ay 8:21; Ebr 13:15Na watoe dhabihu za kushukuru,
na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.