Zaburi 106:40-48 NEN

Zaburi 106:40-48

106:40 Law 26:28; Kut 34:9; 9:29Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake

na akauchukia sana urithi wake.

106:41 Amu 2:14; Neh 9:27Akawakabidhi kwa mataifa

na adui zao wakawatawala.

106:42 Amu 4:3Adui zao wakawaonea

na kuwatia chini ya mamlaka yao.

106:43 Amu 7:1-25; 2:16-19; 6:1-7; Yos 10:14; Neh 9:28Mara nyingi aliwaokoa

lakini walikuwa wamezama kwenye uasi,

nao wakajiharibu katika dhambi zao.

106:44 Amu 3:9; 10:10Lakini akaangalia mateso yao

wakati aliposikia kilio chao;

106:45 Mwa 9:15; Lk 1:72; Za 105:8; 103:11; 17:7; Law 26:41; Mao 3:32; Kut 32:14kwa ajili yao akakumbuka agano lake,

na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.

106:46 1Nya 16:8; Mt 19:17; 2Nya 5:13; 7:3Akawafanya wahurumiwe

na wote waliowashikilia mateka.

106:47 Za 147:2; 105:1; 30:4; 99:3; 28:9; 107:3; Isa 11:12; 27:13; 56:8; 66:20; Yer 31:8; Lk 1:74; Eze 20:34; Mik 4:6; 2Kor 5:15Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe.

Tukusanye tena kutoka kwa mataifa,

ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu,

na kushangilia katika sifa zako.

106:48 Za 41:13; 72:19Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli,

tangu milele na hata milele.

Watu wote na waseme, “Amen!”

Msifuni Bwana.

Read More of Zaburi 106