Zaburi 105:37-45 NEN

Zaburi 105:37-45

105:37 Kut 3:21, 22Akawatoa Israeli katika nchi

wakiwa na fedha na dhahabu nyingi,

wala hakuna hata mmoja

kutoka kabila zao aliyejikwaa.

105:38 Kut 15:16Misri ilifurahi walipoondoka,

kwa sababu hofu ya Israeli ilikuwa imewaangukia.

105:39 Kut 13:21; 1Kor 10:1; Za 78:14; Neh 9:12Alitandaza wingu kama kifuniko,

na moto kuwamulikia usiku.

105:40 Za 78:18; Kut 16:4; Yn 6:31; Kut 16:12Waliomba, naye akawaletea kware,

akawashibisha kwa mkate wa mbinguni.

105:41 Hes 20:11; 1Kor 10:4; Kut 17:6; Neh 9:15; Isa 48:21Alipasua mwamba, maji yakabubujika,

yakatiririka jangwani kama mto.

105:42 Mwa 15:1-4, 13-16; 13:14-17Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu,

aliyompa Abrahamu mtumishi wake.

105:43 Kut 15:1-19; Za 106:12Aliwatoa watu wake kwa furaha,

wateule wake kwa kelele za shangwe,

105:44 Kum 6:10-11; Za 106:12akawapa nchi za mataifa, wakawa warithi

wa mali wengine walikuwa wameitaabikia:

105:45 Kum 6:14-21; 4:1, 40; Za 105:35; 78:5-7alifanya haya ili wayashike mausia yake

na kuzitii sheria zake.

Msifuni Bwana.105:45 Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.

Read More of Zaburi 105